chikita

TANGAZA NASI

Wednesday, August 10, 2011

WAFANYA BIASHARA WA MAFUTA WAMEPOKEAJE BITI LA WANENE?

“Hili ni tatizo kubwa, lazima Serikali ionyeshe ipo na ina uwezo wa kusimamia, watu sasa wananunua kwa mfano, Korogwe lita moja ya mafuta ni Sh3,000, Handeni Sh4, 000 naambiwa Tabora hakuna kabisa mafuta... hili ni jambo la hatari kwa usalama wa nchi,” alisema Makamba na kuongeza:Tunataka kuiona hali ya mafuta inarejea kama ilivyokuwa awali, kama tutashindwa kufanya uamuzi, nchi itasimama, wananchi hawatuelewi. Chama Cha Mapinduzi (CCM), ndicho kimeunda Serikali, lakini suala hili la mafuta linavyofanyika sivyo wananchi walivyotegemea. Mheshimiwa Waziri sema kitu, Mheshimiwa Waziri Mkuu sema kitu, kwa sababu ipo Ewura lakini Serikali ipo, haiwezekani siku saba nzima hatujasikia Waziri Mkuu amesema kitu, wala Waziri amesema kitu kwa nini? Hili jambo baya, tunaomba muonyeshe mpo na mnafanya kazi............." januari makamba

wafanyabiashara hao waagizwe kufungua vituo vya mafuta na kuendelea kutoa huduma mara moja na kwamba kama hawatafanya hivyo hadi jana saa 12:00 jioni, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ), livifungue na kuyauza kwa nguvu. Alisema katika hali ya kawaida imezoeleka kuona wanaogoma ni wafanyakazi na hajawahi kutokea wafanyabiashara wakagoma: “Hatujasikia wafanyabiashara wamekata rufani tangu kushushwa bei au wamekwenda Tume ya Ushindani (FCC) kukata rufani. Wanataka kutuonyesha ubabe wao, wanataka kutumia jeuri ya fedha, Watanzania siku zote ni maskini jeuri, leo mafuta yatoke, Ewura waagize yatoke ikifika saa 12 jioni wamegoma basi wanyang’anywe leseni mara moja  na JWTZ liingie na wafungue vituo mafuta yatoke.”..........." kabwe zito